ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُم بِٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ فَلَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Wale wanao toa mali zao usiku na mchana, kwa siri na dhaahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wale ambao wanatoa mali zao kwa kumridhisha Mwenyezi Mungu, mchana na usiku, kwa siri na kwa dhahiri, watapata malipo yao mbele ya Mola wao, na wala hapana khofu juu yao kuhusu mambo watakayoyakabili Akhera wala hawatakuwa na huzuni juu ya vitu vya kidunia vilivyowapita wasivipate. Sheria hiyo ya Ki- Mungu yenye hekima, ndiyo njia ya Uislamu katika utoaji, yenye kuondoa mahitaji ya mafukara kwa heshima na utu, kusafisha mali ya matajiri na kuhakikisha kusaidiana juu ya wema na ucha-Mungu ili kutaka radhi za Mwenyezi Mungu bila maonevu au kulazimisha.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس