هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ لَكُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰٓ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَسَوَّىٰهُنَّ سَبۡعَ سَمَٰوَٰتٖۚ وَهُوَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Yeye ndiye aliye kuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi. Tena akazielekea mbingu, na akazifanya mbingu saba. Naye ndiye Mjuzi wa kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Ndiye Aliyeumba kwa ajili yenu kila kilichoko kwenye ardhi miongoni mwa neema ambazo mnanufaika nazo, kisha Akaelekea na kukusudia kuumba mbingu, Akazifanya mbingu saba. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kitu, na elimu Yake, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, imevizunguka vitu vyote Alivyoviumba.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس