قَالُواْ ٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا لَوۡنُهَاۚ قَالَ إِنَّهُۥ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٞ صَفۡرَآءُ فَاقِعٞ لَّوۡنُهَا تَسُرُّ ٱلنَّـٰظِرِينَ
Wakasema: Tuombee kwa Mola wako atupambanulie nini rangi yake? Akasema: Yeye anasema, kuwa ng'ombe huyo ni wa manjano, na rangi yake imekoza, huwapendeza wanao mtazama.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wakarudi kwenye kujadili kwao wakisema, “Mwambie Mola wako Atufafanulie rangi yake.” Akasema kuwaambia, “Yeye anasema kwamba huyo ni rangi ya manjano iliyoiva sana, anayemtia furaha mwenye kumwangalia.”
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس