وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Na wale walio amini na wakatenda mema, hao ndio watu wa Peponi, humo watadumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hukumu ya Mwenyezi Mungu iliyothibiti, kwa upande mwengine, ni kwamba wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake imani ya kikweli iliyosafika na Wakafanya vitendo vinavyoambatana na Sheria ya Mwenyezi Mungu Aliyowapelekea Mitume Wake kwa njia ya Wahyi, hao watakaa Peponi makao ya milele yasiyokatika huko Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس