۞وَلَقَدۡ جَآءَكُم مُّوسَىٰ بِٱلۡبَيِّنَٰتِ ثُمَّ ٱتَّخَذۡتُمُ ٱلۡعِجۡلَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَنتُمۡ ظَٰلِمُونَ
Na alikufikieni Musa na hoja zilizo waziwazi, kisha mkamchukua ndama (kumuabudu) baada yake, na mkawa wenye kudhulumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika Nabii wa Mwenyezi Mungu, Mūsā, aliwajia nyinyi na miujiza iliyo wazi yenye dalili ya ukweli wake, kama mafuriko, nzige, chawa, vyura na mengineyo katika yale aliyoyataja Mwenyezi Mungu katika Qur’ani tukufu. Pamoja na hivyo, mumemchukuwa ndama mkamfanya ni muabudiwa, baada ya Mūsā kuondoka kuenda kukutana na Mola wake. Na nyinyi kwa kufanya hivyo mnavuka mipaka ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس