وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ نَافِلَةٗۖ وَكُلّٗا جَعَلۡنَا صَٰلِحِينَ
Naye tukampa Is-haq, na Yaaqub kuwa ni ziada. Na wote tukawajaalia wawe watu wema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Alimneemesha Ibrāhīm kwa kumtunuku Isḥāq alipomuomba, na zaidi ya hilo Alimtunuku, kutokana na Isḥāq, Ya'qūb. Na kila mmoja kati ya Ibrāhīm na Isḥāq na Ya'qūb Mwenyezi Mungu Alimjaalia kuwa mwema na mtiifu Kwake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس