وَٱلۡوَزۡنُ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡحَقُّۚ فَمَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Na Siku hiyo kipimo kitakuwa kwa Haki. Basi watakao kuwa na uzani mzito, hao ndio watakao fanikiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kuvipima vitendo vya watu Siku ya Kiyama kutakuwa ni kwa mizani ya kikweli, kwa usawa na uhaki ambao hauna maonevu. Basi yoyote yule ambaye mizani za vitendo vyake zitakuwa nzito, kwa wingi wa mema yake, hao ndio watakaofaulu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس