ترجمة معاني سورة الشمس باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭜﭝ
ﭞ
As-Shams
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
آية رقم 2
ﭟﭠﭡ
ﭢ
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
آية رقم 3
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
آية رقم 4
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na kwa usiku unapo lifunika!
آية رقم 5
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
آية رقم 6
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
آية رقم 7
ﭳﭴﭵ
ﭶ
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
آية رقم 8
ﭷﭸﭹ
ﭺ
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
آية رقم 9
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
آية رقم 10
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
آية رقم 11
ﮅﮆﮇ
ﮈ
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
آية رقم 12
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
آية رقم 13
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
آية رقم 14
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
آية رقم 15
ﮝﮞﮟ
ﮠ
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
تقدم القراءة