ترجمة سورة الضحى

Ali Muhsin Al - Swahili translation
ترجمة معاني سورة الضحى باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation .

Ad-Dhuhah


Naapa kwa mchana!

Na kwa usiku unapo tanda!

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

Basi yatima usimwonee!

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Icon