وَلَوۡ أَنَّهُمۡ ءَامَنُواْ وَٱتَّقَوۡاْ لَمَثُوبَةٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ خَيۡرٞۚ لَّوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Na lau kuwa wangeamini na wakaogopa, bila ya shaka malipo yatokayo kwa Mwenyezi Mungu yange kuwa bora. Laiti wangeli kuwa wanajua!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau Mayahudi waliamini na kumuogopa Mwenyezi Mungu, wangalikuwa na yakini kuwa thawabu za Mwenyezi Mungu ni bora kwao kuliko uchawi na kuliko yale waliyoyapata kupitia huo uchawi. Lau walikuwa wanajua thawabu na malipo yanayopatikana kwa kuamini na kumcha Mwenyezi Mungu, ujuzi wa kihakika, wangaliamini.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس