مَّا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَلَا ٱلۡمُشۡرِكِينَ أَن يُنَزَّلَ عَلَيۡكُم مِّنۡ خَيۡرٖ مِّن رَّبِّكُمۡۚ وَٱللَّهُ يَخۡتَصُّ بِرَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ
Walio kufuru miongoni mwa watu wa Kitabu na washirikina hawapendi mteremshiwe kheri yoyote kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Na Mwenyezi Mungu humkusudia kumpa rehema yake ampendaye. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Makafiri, miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina, hawapendi mteremshiwe kheri, hata kama ni ndogo kabisa, itokao kwa Mola wenu, iwe ni Qur’ani au elimu au ushindi au bishara njema. Mwenyezi Mungu Anamhusisha Amtakaye kwa rehema Zake za unabii na utume. Mwenyezi Mungu ni Mwenye vipaji vingi venye kuenea.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس