يَٰبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتِيَ ٱلَّتِيٓ أَنۡعَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ وَأَنِّي فَضَّلۡتُكُمۡ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni neema yangu niliyo kuneemesheni, na hakika Mimi nikakufadhilisheni kuliko wengineo wote.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi kizazi cha Ya’qūb, tajeni neema zangu kubwa kwenu na mkumbuke kuwa niliwatukuza juu ya watu wa zama zenu kwa wingi wa Manabii wenu na kwa Vitabu walivyoteremshiwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس