إِذۡ تَبَرَّأَ ٱلَّذِينَ ٱتُّبِعُواْ مِنَ ٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُواْ وَرَأَوُاْ ٱلۡعَذَابَ وَتَقَطَّعَتۡ بِهِمُ ٱلۡأَسۡبَابُ
Walio fuatwa watakapo wakataa wale walio wafuata, na hali ya kuwa wamekwisha iona adhabu; na yatakatika mafungamano yao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Watakapoiyona adhabu ya Akhera, watajitenga wale viongozi waliofuatwa kujiepusha na wale waliowafuata katika ushirikina na zitawakatikia wao aina zote za mawasiliano waliyojifungamanisha nayo duniani: ya ujamaa, ufuasi, dini na mengineyo yasiyokuwa hayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس