وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَشۡرِي نَفۡسَهُ ٱبۡتِغَآءَ مَرۡضَاتِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ رَءُوفُۢ بِٱلۡعِبَادِ
Na katika watu yupo ambaye huiuza nafsi yake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na baadhi ya watu huziuza nafsi zao kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu, kwa kupigana jihadi katika njia Yake na kujilazimisha kumtii. Na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja, Anawarehemu waja wake Waumini rehema kunjufu, katika ulimwengu wao na Akhera yao, na kuwalipa malipo mazuri zaidi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس