إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱلَّذِينَ هَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أُوْلَـٰٓئِكَ يَرۡجُونَ رَحۡمَتَ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Hakika wale walio amini na wale walio hama na wakapigania Njia ya Mwenyezi Mungu, hao ndio wanao taraji rehema za Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale ambao walimuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakazitumia Sheria zake, wale waioyaacha Makaazi yao na wakapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, hao ni wenye kutaraji kupata fadhila za Mwenyezi Mungu na thawabu Zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasamehe madhambi ya waja Wake Waumini, ni Mwenye kuwarehemu rehema kunjufu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس