ٱللَّهُ وَلِيُّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يُخۡرِجُهُم مِّنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِۖ وَٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَوۡلِيَآؤُهُمُ ٱلطَّـٰغُوتُ يُخۡرِجُونَهُم مِّنَ ٱلنُّورِ إِلَى ٱلظُّلُمَٰتِۗ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Mwenyezi Mungu ni Mlinzi wa walio amini. Huwatoa gizani na kuwaingiza mwangazani. Lakini walio kufuru, walinzi wao ni Mashet'ani. Huwatoa kwenye mwangaza na kuwaingiza gizani. Hao ndio watu wa Motoni, na humo watadumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Anawasimamia Waumini kwa kuwanusuru, kuwaafikia na kuwahifadhi, Anawatoa kutoka kwenye magiza ya ukafiri kuwapeleka kwenye nuru ya Imani. Na wale waliokufuru, wanusuru wao na wasaidizi wao ni wale wafananishwao na Mwenyezi Mungu na masanamu wanaowaabudu wasiokuwa Mwenyezi Mungu. Hao wanawatoa wao kutoka kwenye nuru ya Imani kuwapeleka kwenye magiza ya ukafiri. Wao ndio watu wa Motoni wenye kutindikia humo, wenye kusalia humo milele na si wenye kutoka humo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس