يَمۡحَقُ ٱللَّهُ ٱلرِّبَوٰاْ وَيُرۡبِي ٱلصَّدَقَٰتِۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ كَفَّارٍ أَثِيمٍ
Mwenyezi Mungu huiondolea baraka riba, na huzibariki sadaka. Na Mwenyezi Mungu hampendi kila mwenye kukanya na afanyae dhambi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Anaiyondoa riba yote au Anamnyima mlaji riba baraka ya mali yake asinufaike nayo. Na Anazikuza sadaka na kuzifanya ziwe nyingi na Anawaongezea malipo wenye kutoa sadaka maradufu na Anawabarikia katika mali yao. Na Mwenyezi Mungu Hampendi kila mwenye kushikilia kwenye ukafiri wake, mwenye kujihalalishia ulaji riba, mwenye kukolea nadani ya dhambi na haramu na kumuasi Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس