فَجَعَلۡنَٰهَا نَكَٰلٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهَا وَمَا خَلۡفَهَا وَمَوۡعِظَةٗ لِّلۡمُتَّقِينَ
Kwa hivyo tukayafanya hayo kuwa onyo kwa wale walio kuwa katika zama zao na walio kuja baada yao, na mawaidha kwa wachamngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Tukakifanya kijiji hicho ni mazingatio kwa watu wa vijiji vya karibu ambao itawafikia habari yake na vituko vilivyotokea huko, na ni mazingatio kwa mwenye kufanya madhambi kama hayo baada yake. Na pia tulikifanya ni mawaidha kwa watu wema, wapate kujua kuwa wao wako kwenye haki, ili wasimame imara juu yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس