قُلۡ إِن كَانَتۡ لَكُمُ ٱلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ عِندَ ٱللَّهِ خَالِصَةٗ مِّن دُونِ ٱلنَّاسِ فَتَمَنَّوُاْ ٱلۡمَوۡتَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Sema: Ikiwa nyumba ya Akhera iliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni yenu tu bila ya watu wengine, basi tamanini mauti kama nyinyi mnasema kweli.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, kuwaambia Mayahudi ambao wanadai kuwa Pepo ni yao peke yao, kwa kudai kuwa wao tu, bila watu wengine, ndio mawalii wa Mwenyezi Mungu na kuwa wao ni watoto Wake na vipenzi Vyake, “Mambo yakiwa ni hivyo, waapizeni kufa waliyo warongo katika nyinyi au wasiokuwa katika nyinyi, iwapo nyinyi ni wakweli katika madai yenu haya.”
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس