Al-Anbiya
ٱقۡتَرَبَ لِلنَّاسِ حِسَابُهُمۡ وَهُمۡ فِي غَفۡلَةٖ مُّعۡرِضُونَ
IMEWAKARIBIA watu hisabu yao, nao wamo katika mghafala wanapuuza.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Umekaribia wakati wa kuhesabiwa watu juu ya matendo waliyoyatanguliza, pamoja na hivyo, makafiri wanaishi wakiwa kwenye hali ya kupumbaa, wameghafilika na uhakika huu, wakiwa kwenye hali ya kulipa mgongo onyo hili.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس