لَهُمۡ فِيهَا زَفِيرٞ وَهُمۡ فِيهَا لَا يَسۡمَعُونَ
Lao wao humo ni kupiga mayowe, na wala hawatasikia (jenginelo).
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa wenye kuadhibiwa Motoni wataona uchungu unaooneshwa na mlio wa sauti zao ambapo pumzi zao zinatoka kwa nguvu sana kutoka kwenye vifua vyao. Na wao wakiwa Motoni hawasikii kwa ukali wa adhabu wanayopewa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس