وَلَئِن مُّتُّمۡ أَوۡ قُتِلۡتُمۡ لَإِلَى ٱللَّهِ تُحۡشَرُونَ
Na mkifa au mkiuliwa ni kwa Mwenyezi Mungu ndio mtakusanywa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na iwapo ajali zenu zitakoma katika haya maisha ya dunia na mkafa juu ya matandiko yenu au mkauawa katika uwanja wa mapigano, ni kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Mtakusanywa; na huko Atawalipa kwa matendo yenu mliyoyatenda.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس