فَنَادَتۡهُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَهُوَ قَآئِمٞ يُصَلِّي فِي ٱلۡمِحۡرَابِ أَنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكَ بِيَحۡيَىٰ مُصَدِّقَۢا بِكَلِمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَسَيِّدٗا وَحَصُورٗا وَنَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Alipo kuwa kasimama chumbani akisali, Malaika kamnadia: Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria Yahya, ataye kuwa mwenye kusadikisha neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu, na ni bwana na mt'awa na Nabii kwa watu wema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hapo Malaika walimuita, naye yuko katika hali ya kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu katika mahali pake pa Swala, huku anamuomba Yeye, wakamuambia. «Mwenyezi Mungu Anakupa habari yenye kukufurahisha, nayo ni kwamba utaruzukiwa mtoto ambaye jina lake ni Yaḥyā, ambaye atalisadikisha neno la Mwenyezi Mungu, naye ni 'Īsā mwana wa Maryam, amani imshukie. Huyo Yaḥyā atakuwa ni bwana wa kaumu yake, atakuwa na cheo na daraja kubwa, atakuwa ni mwenye kujihifadhi: hatendi madhambi wala hafuati matamanio ya kudhuru na atakuwa ni Nabii miongoni mwa watu wema ambao walifikia kilele cha wema.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس