وَجَٰوَزۡنَا بِبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱلۡبَحۡرَ فَأَتَوۡاْ عَلَىٰ قَوۡمٖ يَعۡكُفُونَ عَلَىٰٓ أَصۡنَامٖ لَّهُمۡۚ قَالُواْ يَٰمُوسَى ٱجۡعَل لَّنَآ إِلَٰهٗا كَمَا لَهُمۡ ءَالِهَةٞۚ قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٞ تَجۡهَلُونَ
Na tukawavusha bahari Wana wa Israili, wakafika kwa watu wanao abudu masanamu yao. Wakasema: Ewe Musa! Hebu tufanyie na sisi miungu kama hawa walivyo kuwa na miungu. Musa akasema: Hakika nyinyi ni watu msio jua kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na tuliwakatia Wana wa Isrāīl bahari, wakapita kwa watu waliokuwa wamekaa na kuendelea kuabudu masanamu wao. Wana wa Isrāīl wakasema, «Tufanyie, ewe Mūsā, sanamu tupate kumuabudu na kumfanya mungu kama hawa watu walivyo na masanamu wanaowaabudu.» Mūsā akawaambia, «Hakika yenu nyinyi,enyi watu, ni wajinga wa kujua utukufu wa Mwenyezi Mungu, na hamjui kwamba ibada haifai kufanyiwa yoyote isipokuwa Mwenyezi Mungu, Aliye Mmoja, Mwenye kutendesha nguvu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس