فَأَنجَيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ
Basi tukamwokoa yeye na watu wake, isipo kuwa mkewe, alikuwa miongoni mwa walio bakia nyuma.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi Mwenyezi Mungu Akamuokoa Lūṭ, na wafuasi wake na adhabu, Alimuamuru auhame mji ule, isipokuwa mke wake, kwani yeye alikuwa ni miongoni mwa walioangamia, waliosalia ndani ya adhabu ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس