ترجمة معاني سورة الفجر باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭤ
ﭥ
Al-Fajr
Naapa kwa alfajiri,
آية رقم 2
ﭦﭧ
ﭨ
Na kwa masiku kumi,
آية رقم 3
ﭩﭪ
ﭫ
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
آية رقم 4
ﭬﭭﭮ
ﭯ
Na kwa usiku unapo pita,
آية رقم 5
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
آية رقم 6
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
آية رقم 7
ﭾﭿﮀ
ﮁ
Wa Iram, wenye majumba marefu?
آية رقم 8
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
آية رقم 9
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
آية رقم 10
ﮏﮐﮑ
ﮒ
Na Firauni mwenye vigingi?
آية رقم 11
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
آية رقم 12
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Wakakithirisha humo ufisadi?
آية رقم 13
ﮜﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
آية رقم 14
ﮢﮣﮤ
ﮥ
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
آية رقم 15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
آية رقم 16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
آية رقم 17
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
ﯤ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
آية رقم 18
ﯥﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Wala hamhimizani kulisha masikini;
آية رقم 19
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
آية رقم 20
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
آية رقم 21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
آية رقم 22
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
آية رقم 23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
آية رقم 24
ﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
آية رقم 25
ﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
آية رقم 26
ﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
آية رقم 27
ﭬﭭﭮ
ﭯ
Ewe nafsi iliyo tua!
آية رقم 28
ﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
آية رقم 29
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
آية رقم 30
ﭺﭻ
ﭼ
Na ingia katika Pepo yangu.
تقدم القراءة