وَلِلَّهِ ٱلۡمَشۡرِقُ وَٱلۡمَغۡرِبُۚ فَأَيۡنَمَا تُوَلُّواْ فَثَمَّ وَجۡهُ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ
Na mashariki na magharibi ni za Mwenyezi Mungu. Basi kokote mnako elekea, huko Mwenyezi Mungu yupo. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye wasaa na Mjuzi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Zote pande mbili, upande wa kuchomoza jua na wa kutwa kwake na vilivyo baina yake, ni vya Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye Mmiliki wa ardhi yote. Basi pande wowote mnaouelekea kwenye Swala zenu kwa kuwa mmeamrishwa na Mwenyezi Mungu, Hakika nyinyi huwa mnaukusudia Uso Wake, hamkutoka kwenye ufalme Wake na utiifu wenu Kwake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye rehema za kuenea kwa waja Wake, ni Mjuzi wa vitendo vyao, hakuna chochote chenye kufichika Kwake Asikijue.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس