وَقَالُواْ ٱتَّخَذَ ٱللَّهُ وَلَدٗاۗ سُبۡحَٰنَهُۥۖ بَل لَّهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ كُلّٞ لَّهُۥ قَٰنِتُونَ
Na ati wanasema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu! Ametakasika na hayo. Bali vyote viliomo mbinguni na duniani ni vyake. Vyote vinamt'ii Yeye.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na walisema Mayahudi na Wanaswara, “Mwenyezi Mungu Amejifanyia mtoto.” Ameepukana Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa pungufu ni Kwake, na neno hilo la batili! Kwani wote walioko mbinguni na ardhini ni milki Yake na ni watumwa Wake. Wote wanamnyenyekea Yeye na wanapelekewa wakiwa chini ya uendeshaji Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس