فَمَنۢ بَدَّلَهُۥ بَعۡدَ مَا سَمِعَهُۥ فَإِنَّمَآ إِثۡمُهُۥ عَلَى ٱلَّذِينَ يُبَدِّلُونَهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٞ
Na atakaye ubadilisha wasia baada ya kuusikia, basi dhambi yake ni juu ya wale watakao ubadilisha; hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Yule atakaye kuubadilisha wasia wa maiti baada ya kuusikia kutoka kwake kabla hajafariki, dhambi litakuwa ni la yule aliyebadilisha na kugeuza. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuusikia wasia wenu na maneno yenu, ni Mjuzi zaidi wa yale yanayofichwa na nyoyo zenu kuhusu kuelekea upande wa haki na uadilifu au ujeuri na udhalimu, na Atawalipa kwa hilo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس