وَإِذَا قِيلَ لَهُ ٱتَّقِ ٱللَّهَ أَخَذَتۡهُ ٱلۡعِزَّةُ بِٱلۡإِثۡمِۚ فَحَسۡبُهُۥ جَهَنَّمُۖ وَلَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ
Na akiambiwa: Mwogope Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kutenda madhambi. Basi huyo inamtosha Jahannam. Paovu mno hapo kwa mapumziko.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na anaponasihiwa mnafiki huyo mharibifu na akaambiwa, «Mche Mwenyezi Mungu,ujihadhari na adhabu Yake na ukomeke na kuleta uharibifu katika ardhi,» huwa hakubali nasaha. Bali kile kiburi chake na mori wa kijinga humfanya kutenda maovu zaidi. Basi adhabu yenye kumtosheleza yeye na kumkifu ni Jahanamu. Na hakika uovu wa tandiko ndilo hilo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس