لِّلَّذِينَ يُؤۡلُونَ مِن نِّسَآئِهِمۡ تَرَبُّصُ أَرۡبَعَةِ أَشۡهُرٖۖ فَإِن فَآءُو فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Kwa wanao apa kuwa watajitenga na wake zao, wangojee miezi mine. Wakirejea basi Mwenyezi Mungu hakika ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wale wanaoapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba hawatawaingilia wake zao, wana muda wa kusubiriwa wa miezi minne. Iwapo watarudi kabla kumalizika hiyo miezi mine, basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasamehe makosa yaliyofanywa na wao ya kiapo kwa sababu ya kurudi kwao, ni Mwenye huruma nao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس