فَإِنۡ خِفۡتُمۡ فَرِجَالًا أَوۡ رُكۡبَانٗاۖ فَإِذَآ أَمِنتُمۡ فَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ كَمَا عَلَّمَكُم مَّا لَمۡ تَكُونُواْ تَعۡلَمُونَ
Ikiwa mnakhofu (Salini) na hali mnakwenda kwa miguu au mmepanda. Na mtakapo kuwa katika amani, basi mkumbukeni Mwenyezi Mungu kama alivyo kufunzeni yale mliyo kuwa hamyajui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na iwapo mtawaogopa maadui maadui wenu, swalini swala ya khofu, mkiwa mwatembea au mumepanda, kwa namna yoyote ile mnayoiweza, hata kama ishara, au hata kama hamkulekea kibla. Na pindi khofu yenu itakapokwisha, swalini swala ya amani na mumtaje Mwenyezi Mungu humo. Wala msiipunguze kwakuitoa kwenye namna yake ya asili. Na mshukuruni Mwenyezi Mungu kwa kuwafundisha mambo ya ibada na hukumu ambayo hamkuwa na ujuzi nayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس