فَبَدَّلَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ قَوۡلًا غَيۡرَ ٱلَّذِي قِيلَ لَهُمۡ فَأَنزَلۡنَا عَلَى ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ رِجۡزٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ
Lakini walio dhulumu waliibadili kauli isiyo kuwa waliyo ambiwa. Kwa hivyo tukaiteremsha juu ya wale walio dhulumu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya walivyo kuwa wamepotoka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wale wajeuri waliyo wapotevu, katika wana wa Isrāīl, walibadilisha neno la Mwenyezi Mungu na wakaipotoa kauli pamoja na kitendo. Kwani waliingia, na huku wakijikokota kwa matako na wakisema, “habbah fī sha’rah’ (mbegu unyweleni.)”, wakiifanyia maskhara dini ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu Aliwateremshia adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya kuasi kwao na kutoka kwao kwenye utiifu kwa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس