فَجَعَلَهُمۡ جُذَٰذًا إِلَّا كَبِيرٗا لَّهُمۡ لَعَلَّهُمۡ إِلَيۡهِ يَرۡجِعُونَ
Basi akayavunja vipande vipande, ila kubwa lao, ili wao walirudie.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hapo Ibrāhīm akawavunjavunja masanamu akawafanya vipande- vipande vilivyo vidogo na akamuacha mkubwa wao, ili watu wake wapate kumrudia kumuuliza, na ili ulemevu wao na upotevu wao upate kujulikana waziwazi, na ili hoja isimame kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس