أَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا جَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِيَسۡكُنُواْ فِيهِ وَٱلنَّهَارَ مُبۡصِرًاۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Je! Hawaoni kwamba sisi tumeufanya usiku ili watulie, na mchana wa kuangaza. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanao amini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, hawakuona hawa wakanushaji wa aya zetu kwamba sisi tumeufanya usiku ni kipindi cha wao kutulia ndani yake na kulala, na mchana ni kipindi cha wao kuona ili waende kutafuta maisha yao? Hakika katika kuvipelekesha hivyo viwili kuna ushahidi kwa watu wanaoamini ukamilifu wa uweza wa Mwenyezi Mungu, upweke Wake na ukubwa wa neema Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس