وَيَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَفَزِعَ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا مَن شَآءَ ٱللَّهُۚ وَكُلٌّ أَتَوۡهُ دَٰخِرِينَ
Na Siku litapo pulizwa baragumu, watahangaika waliomo mbinguni na katika ardhi, ila amtakaye Mwenyezi Mungu. Na wote watamfikia nao ni wanyonge.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbuka, ewe Mtume, siku ambayo Malaika atakapovuvia kwenye pembe, hapo wababaike walioko mbinguni na ardhini babaiko kubwa sana kwa kituko cha Mvuvio huo, isipokuwa yule aliyevuliwa na Mwenyezi Mungu kati ya wale Aliyowakirimu na Akawahifadhi na hilo babaiko. Na viumbe wote watamjia Mwenyezi Mungu wakiwa wanyonge watiifu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس