أَمۡ نَجۡعَلُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ كَٱلۡمُفۡسِدِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِ أَمۡ نَجۡعَلُ ٱلۡمُتَّقِينَ كَٱلۡفُجَّارِ
Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu kama waovu?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, tuwafanye walioamini wakafanya matendo mema ni kama waharibifu kwenye ardhi? Au je, tuwafanye wachamungu wenye kuamini ni kama waharibifu waliokufuru? Kusawazisha huku hakulingani na hekima ya Mwenyezi Mungu na hukumu yak, kwani hao hawalingani kwa Mwenyezi Mungu. Bali Mwenyezi Mungu Atawalipa wachamungu malipo mema na Atawatesa waharibifu walio waovu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس