ترجمة معاني سورة الليل باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Al-Lail
Naapa kwa usiku unapo funika!
آية رقم 2
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Na mchana unapo dhihiri!
آية رقم 3
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na kwa Aliye umba dume na jike!
آية رقم 4
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
آية رقم 5
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
آية رقم 6
ﯘﯙ
ﯚ
Na akaliwafiki lilio jema,
آية رقم 7
ﯛﯜ
ﯝ
Tutamsahilishia yawe mepesi.
آية رقم 8
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
آية رقم 9
ﯣﯤ
ﯥ
Na akakanusha lilio jema,
آية رقم 10
ﭑﭒ
ﭓ
Tutamsahilishia yawe mazito!
آية رقم 11
ﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
آية رقم 12
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
آية رقم 13
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
آية رقم 14
ﭤﭥﭦ
ﭧ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
آية رقم 15
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Hatauingia ila mwovu kabisa!
آية رقم 16
ﭭﭮﭯ
ﭰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
آية رقم 17
ﭱﭲ
ﭳ
Na mchamngu ataepushwa nao,
آية رقم 18
ﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
آية رقم 19
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
آية رقم 20
ﮀﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
آية رقم 21
ﮆﮇ
ﮈ
Naye atakuja ridhika!
تقدم القراءة