وَلَن تَرۡضَىٰ عَنكَ ٱلۡيَهُودُ وَلَا ٱلنَّصَٰرَىٰ حَتَّىٰ تَتَّبِعَ مِلَّتَهُمۡۗ قُلۡ إِنَّ هُدَى ٱللَّهِ هُوَ ٱلۡهُدَىٰۗ وَلَئِنِ ٱتَّبَعۡتَ أَهۡوَآءَهُم بَعۡدَ ٱلَّذِي جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ مَا لَكَ مِنَ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا نَصِيرٍ
Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao. Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio uwongofu. Na kama ukifuata matamanio yao baada ya ujuzi ulio kwisha kujia, hutapata mlinzi wala msaidizi kwa Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hawataridhika nawe, ewe Mtume, Mayahudi wala Wanaswara isipokuwa ikiwa utaacha Dini yako na ukafuata Dini yao. Waambie, “Dini ya Uislamu ndiyo Dinii sahihi” Na ukifuata matamanio ya hao, baada ya wahyi uliokujia, hutakuwa na rafiki wa kukunufaisha kwa Mwenyezi Mungu wala msaidizi wa kukunusuru. Maneno haya ingawa anaambiwa Mtume, yanalekezwa kwa ummah wote.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس