۞وَإِذِ ٱبۡتَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِـۧمَ رَبُّهُۥ بِكَلِمَٰتٖ فَأَتَمَّهُنَّۖ قَالَ إِنِّي جَاعِلُكَ لِلنَّاسِ إِمَامٗاۖ قَالَ وَمِن ذُرِّيَّتِيۖ قَالَ لَا يَنَالُ عَهۡدِي ٱلظَّـٰلِمِينَ
Na Mola wake Mlezi alipo mjaribu Ibrahim kwa kumpa amri fulani, naye akazitimiza, akamwambia: Hakika Mimi nitakufanya uwe mwongozi wa watu. Akasema: Je, na katika vizazi vyangu pia? Akasema: Ahadi yangu haitawafikia wenye kudhulumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Kumbuka, ewe Nabii, wakati Mwenyezi Mungu Alipomfanyia mtihani Ibrāhīm kwa amri Alizomkalifisha nazo, akazitekeleza na kusimama nazo kwa njia nzuri. Mwenyezi Mungu Akamwambia, “Mimi nimekufanya wewe ni kiigizo kwa watu.” Ibrāhīm akasema, “Ewe Mola wajaalie baadhi ya watu wa kizazi chake ni viongozi kwa ukarimu Zako.” Mwenyezi Mungu Akamjibu kwamba madhalimu hawatapata uongozi wa kidini.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس