وَأَنفِقُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَلَا تُلۡقُواْ بِأَيۡدِيكُمۡ إِلَى ٱلتَّهۡلُكَةِ وَأَحۡسِنُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamizo. Na fanyeni wema. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na endeleeni, enyi Waumini, kutoa mali kwa kuinusuru dini ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na kupigana jihadi katika njia yake. Wala msiziingize nafsi zenu kwenye maangamivu kwa kuacha jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na kuacha kutoa katika njia Yake. Na fanyeni wema katika kutoa na kutii, na mzifanye amali zenu zote ni zenye kutakasika kwa kukusudiwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. Kwa hakika Mwenyezi Mungu Anawapenda watu wenye kutakasa nia na kufanya wema.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس