وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَكُمۡ وَرَفَعۡنَا فَوۡقَكُمُ ٱلطُّورَ خُذُواْ مَآ ءَاتَيۡنَٰكُم بِقُوَّةٖ وَٱذۡكُرُواْ مَا فِيهِ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Na tulipo chukua ahadi yenu, na tukaunyanyua mlima juu yenu (tukakwambieni): Shikeni kwa nguvu haya tuliyo kupeni, na yakumbukeni yaliyomo ndani yake ili mpate kujilinda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbukeni, enyi Wana wa Isrāīl, tulipochukua kutoka kwenu ahadi ya mkazo ya kumuamini Mwenyezi Mungu na kumpwekesha kwa ibada, na tukaliinua jabali la Tūr juu yenu na tukawaambia, “Chukueni, kwa bidii na jitihadi, Kitabu tulichowapa na mkitunze. Na mkitofanya hivyo, tutaliangusha hili jabali juu yenu liwafinike, na msiisahau Taurati kwa maneno na vitendo, mpate kunicha na kuiogopa adhabu Yangu.”
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس