فَأَنجَيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَٰهَا مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe; tukamkadiria katika walio baki nyuma.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Tukamuokoa Lūṭ na watu wake waliomfuata na adhabu ambayo itawashukia watu wa Lūṭ waliomkanusha, isipokuwa mkewe tuliomkadria kuwa ni mwenye kusalia kwenye adhabu mpaka aangamie pamoja na wenye kuangamia, kwa kuwa yeye alikuwa ni msaidizi wa watu wake kwa matendo yao mabaya na alikua akiridhika nayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس