وَعَجِبُوٓاْ أَن جَآءَهُم مُّنذِرٞ مِّنۡهُمۡۖ وَقَالَ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا سَٰحِرٞ كَذَّابٌ
Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wameona ajabu washirikina hawa kuwa Mwenyezi Mungu Amewatumia binadamu miongoni mwao awalinganie kwa Mwenyezi Mungu na awaogopeshe adhabu Yake na wakasema, «Hakika yeye si Mtume bali yeye ni mrongo katika maneno yake, anawafanyia uchawi watu wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس