صُمُّۢ بُكۡمٌ عُمۡيٞ فَهُمۡ لَا يَرۡجِعُونَ
Viziwi, mabubu, vipofu; kwa hivyo hawatarejea.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wao ni viziwi, hawaisikii haki kwa kuizingatia, ni mabubu, hawaitamki haki, ni vipofu, hawauoni mwangaza wa uongofu. Kwa hivyo, hawawezi kurudi kwenye Imani ambayo waliiacha na kuchukuwa upotevu badali yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس