وَلَا تَجۡعَلُواْ ٱللَّهَ عُرۡضَةٗ لِّأَيۡمَٰنِكُمۡ أَن تَبَرُّواْ وَتَتَّقُواْ وَتُصۡلِحُواْ بَيۡنَ ٱلنَّاسِۚ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٞ
Wala msifanye jina la Mwenyezi Mungu katika viapo vyenu kuwa ni kisingizio cha kuacha kufanya wema na kuchamngu na kupatanisha baina ya watu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wala msikifanye, enyi Waislamu, kiapo chenu kwa Mwenyezi Mungu kuwa ni chenye kuwazuia nyinyi kufanya wema, kuunga kizazi, kumcha Mwenyezi Mungu na kusuluhisha kati ya watu. Nako ni iwapo mtaitwa kufanya lolote katika hayo, mkakataa na kutoa hoja kwamba mliapa kwa Mwenyezi Mungu kuwa hamtalifanya. Bali ni juu ya Mwenye kuapa ageuze kiapo chake, afanye vitendo vya kheri na atoe kafara ya kiapo chake wala asizowee jambo hilo. Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasikia maneno yenu, ni Mwenye kuzijua hali zenu zote.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس