وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّ أَرِنِي كَيۡفَ تُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰۖ قَالَ أَوَلَمۡ تُؤۡمِنۖ قَالَ بَلَىٰ وَلَٰكِن لِّيَطۡمَئِنَّ قَلۡبِيۖ قَالَ فَخُذۡ أَرۡبَعَةٗ مِّنَ ٱلطَّيۡرِ فَصُرۡهُنَّ إِلَيۡكَ ثُمَّ ٱجۡعَلۡ عَلَىٰ كُلِّ جَبَلٖ مِّنۡهُنَّ جُزۡءٗا ثُمَّ ٱدۡعُهُنَّ يَأۡتِينَكَ سَعۡيٗاۚ وَٱعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ
Na alipo sema Ibrahim: Mola wangu Mlezi! Nionyeshe vipi unavyo fufua wafu. Mwenyezi Mungu akasema: Kwani huamini? Akasema: Hasha! Lakini ili moyo wangu utue. Akamwambia: Twaa ndege wane na uwazoeshe kwako, kisha uweke juu ya kila kilima sehemu, kisha wete, watakujia mbio. Na ujue kwamba hakika Mwenyezi Mungu ni Mtukufu Mwenye nguvu, na Mwenye hikima.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Kumbuka, ewe Mtume, maombi ya Ibrahim kwa Mola wake Amuoneshe namna ya Ufufuzi. Mwenyezi Mungu Alimwambia, «Kwani huamini?» Akasema, «La! Nakuamini. Lakini nataka hilo ili nipate yakini zaidi juu ya yakini niliyonayo.» Akasema, «Chukua ndege wanne, uwe nao, uwachinje na uwakatekate kisha weka sehemu ya hao ndege juu ya kila jabali. Kisha waite, watakujia kwa haraka.» Ibrahim, amani imshukie, akawita. Papo hapo kila sehemu ikarudi mahali pake, na papo hapo wakamjia kwa haraka. Na ujue kuwa Mwenyezi Mungu ni Mshindi, hakuna kimshindacho, ni Mwenye hekima katika maneno Yake, vitendo Vyake, sheria Yake na makadirio Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس