حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءُو قَالَ أَكَذَّبۡتُم بِـَٔايَٰتِي وَلَمۡ تُحِيطُواْ بِهَا عِلۡمًا أَمَّاذَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Hata watakapo fika, atasema (Mwenyezi Mungu): Je! Nyinyi si mlizikanusha Ishara zangu pasipo kuzijua vyema? Au mlikuwa mkifanya nini?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mpaka litakapokuja, miongoni mwa kila jamii, pote la wale wanaozikanusha aya zetu na wakakusanyika, Mwenyezi Mungu Atasema, «Je, mumezikanusha aya zangu nilizoziteremsha kwa Mitume wangu na alama nilizozisimamisha zenye kuonyesha upweke wangu na ustahiki wangu peke yangu kuabudiwa na hali nyinyi hamkuwa na ujuzi wa kutosha kuwa ni batilifu, hata iwafanye mzipe mgongo na mzikanushe au ni kitu gani mlikuwa mkifanya?»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس