وَتَرَى ٱلۡجِبَالَ تَحۡسَبُهَا جَامِدَةٗ وَهِيَ تَمُرُّ مَرَّ ٱلسَّحَابِۚ صُنۡعَ ٱللَّهِ ٱلَّذِيٓ أَتۡقَنَ كُلَّ شَيۡءٍۚ إِنَّهُۥ خَبِيرُۢ بِمَا تَفۡعَلُونَ
Na unaiona milima unaidhunia imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu. Huo ndio ufundi wa Mwenyezi Mungu aliye tengeneza vilivyo kila kitu. Hakika Yeye anazo khabari za yote myatendayo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na utayaona majabali ukidhania kuwa yamesimama na yametulia na hali yanatembea mwendo wa kasi kama vile yanavyotembea mawingu yanayopelekwa na upepo. Na huu ni katika utengenezaji wa Mwenyezi Mungu Ambaye Ametengeneza uumbaji wa kila kitu na Akaufanya mzuri madhubuti. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi wa mnayoyafanya, enyi watu, yawe mazuri au mabaya na Atawalipa kwa hayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس