ترجمة معاني سورة المزّمّل باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒ
ﭓ
Al-Muzzammil
Ewe uliye jifunika!
آية رقم 2
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!
آية رقم 3
ﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Nusu yake, au ipunguze kidogo.
آية رقم 4
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.
آية رقم 5
ﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.
آية رقم 6
Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.
آية رقم 7
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.
آية رقم 8
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.
آية رقم 9
Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.
آية رقم 10
Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.
آية رقم 11
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!
آية رقم 12
ﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!
آية رقم 13
ﮡﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.
آية رقم 14
Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!
آية رقم 15
Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.
آية رقم 16
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.
آية رقم 17
Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
آية رقم 18
Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.
آية رقم 19
Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.
آية رقم 20
Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
تقدم القراءة